Katika mwendelezo wa Maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani (MASIKIDU) mwaka 2025, Kiswahili kimeendelea kupewa msukumo katika jukwaa la kimataifa kupitia ushirikiano wa kimkakati kati ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), taasisi za kitaifa na kimataifa, na wadau wa sekta binafsi.